Taarifa kamili: Ajali mbaya ya Lori lamafuta singida.

Ajali mbaya ime tokea mkoani Singida ambapo lori la mafuta limeanguka na kuwaka moto katika eneo la Mlima Sekenke na watu wawili wanaripotiwa kufariki. -RPC Singida Deborah Magiligimba amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo. RPC Singida Deborah Magiligimba amesema kwamba, ajali hiyoimetokea saa nne na nusu asubuhi milima ya Senkenke Wilaya ya Iramba barabara ya Singida - Nzega. Aja li iliyo husisha Gari lenye namba T167 DTC aina ya Flight liner ambayo ilikuwa na Trailer namba T 960 ALS. Hili gari ni mali ya Petromac Africa Dar es salaam. Gali iliacha njia na kupinduka ambapo ililipuka na kusababisha moto mkubwa uliopelekea vifo vya watu wawili ambao ni wanaume. Uchunguzi wa jeshi la Polisi wa awali baada ya kufatilia kwenye mzani wa Singida, gari ilipimwa mzani wa Singida saa moja na dk 27 asubuhi dereva alikua anaitwa Erasto Abedi Rusazi na alikuwa na tingo msaidizi wake anayeitwa Ramadhani Hashim Ramadhini wote ni Wakazi wa Tabata Dar Es Salaam. RPC Deborah Magiligimba, ametoa wito kwa madereva watii sharia za barabarani ili kuepusha ajali.

Comments

Popular posts from this blog

BASI LINGINE LA NEW FORCE LAPATA AJALI MBAYA.

DEATH OF JOHN RAMBO IS IT TRUE

DALILI 10 ZA KUACHA NA MPENZI WAKO